Ay na Fa ndani X bongo nite
Mkali wa Falsafa na mkali wa staili walipokutana jukwaa moja, yaani Ambwene Yesaya ‘Ay’ na Hamisi Mwijuma ‘Fa’, hakika ilikuwa buludani ya aina yake katika usiku wa X BONGO NITE, pale New maisha club kwani walitoa buludani ya nguvu, huku mwana Fa akiutangaza rasmi wimbo wake mpya ukija kwenye video wa Unanijua Unanisikia.
Mwana Fa pia alisema video yake ataanza kuisambaza hivi karibuni, ambayo anaomba mashabiki wake waingoje kwa hamu.
Ay akisababisha, katika ukumbi wa New Maisha
Wakati Ay na Fa wakiimba, ndipo akapanda bonge mmoja na kuanza kukata mauno huku akicheza, huazi amini jinsi alivyokuwa na kitambi na alivyoweza kucheza
B 12 wa XXL pale Clouse Fm, kwenye mjengo wa Mweupe, naye alikuwepo katika show, na hapa akashow love na Bongo5
Hakika kila msanii mkongwe anakuwa na mtu wake anayempenda hasa kwa hawa wasanii wachanga na wanaochipukia kwa kasi, katika siri hizo zilizopo moyoni mwao Mwana Fa, yeye aliivunja siri yake kwa kusema katika wasanii wanaokuja kwa kasi, anaowapenda ni wawili.
Wa kwanza kijana toka Morogoro, Belle 9, na kijana mwingine toka Ilala Dar es salaa katika kundi la Dar Stamina , Shetter
Stive ‘Dj Skills’ na Jaffarai wakiwa kwenye pozi, wakisubiri kuingia kuingia ndani.