Michezo
Azam FC yaiva sasa ipo tayari kuivaa Lipuli
Wachezaji wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, wamefanya mazoezi jioni hii ndani ya Uwanja wa Samora, mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi yao ya kuelekea mchezo wao wa kirafiki kesho Jumatano dhidi ya Lipuli ya huko.
Timu ya wana ramba ramba Azam FC ipo katika ziara yake kwaajili ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi pamoja na michuano mengine mbali mbali.
By Hamza Fumo