Mechi ya shilingi milioni mbili ya waongozaji maarufu wa video nchini, Ijumaa hii (Feb, 7) imefanyika na kuishuhudia timu ya Adam Juma ikibuka na ushindi wa vikapu 81 kwa 74 dhidi ya timu ya Karabani.
Timu ya Adam Juma ikishangilia ushindi na kunyakua shilingi milioni moja
Timu ya Adam Juma iliyokuwa imevalia jezi nyekundu zilizokuwa zimeandikwa ‘Next Level’ ndio ilikuwa ya kwanza kuingia uwanjani hapo kwa mbwembwe nyingi na kuufanya uwanja wa kikapu wa Gymkhana jijini Dar es Salaam kulipuka kwa shangwe kubwa wakati muongozaji huyo maarufu wa video alipokuwa akiingia na kusindikizwa na kundi la wasichana warembo.
Adam Juma akiingia uwanjani
Adam Juma akiwa kwenye benchi lake
Karabani alifuatia kwa kutanguliwa na vijana wa sarakasi waliokuwa wakicheza kwa kufuatiliza wimbo maalum wa Karabani aliotunga kumdiss Adam na huku akiwa amesindikizwa na wasichana warembo wa kizungu.
Karabani na wapambe wake wakiingia uwanjani
Karabani akiwa kwenye benchi lake
Baada mafahari hao kuingia uwanjani hapo, wote kwa pamoja walienda katikati ya uwanja kusalimiana na kupigana vijembe na mikwara pamoja na kutambulisha timu zao.
Huniwezi Wewe: Adam Juma na Karabani wakisalimiana
Nchakalih akionesha kitita kilichoshindaniwa huku Adam Juma akiendelea na majigambo kwa Karabani
MC wa mechi, Nchakalih akiwatambulisha mahasimu kwenye mchezo huo
Picha ya pamoja ya timu ya Adam Juma
Adam Juma akisaliamiana na wachezaji wa timu ya Karabani
Picha ya pamoja ya timu ya Karabani
Mchezaji wa timu ya Karabani
Mechi hiyo ilianza kwa kasi huku timu zote mbili zikionekana kukamiana na kulinda zaidi ngome zao zisishambuliwe na hivyo kufanya magoli mengi yawe ya mitupo ya mbali, lay-ups chache na hakuna dunk hata moja. Kuna wakati mechi ilipwaya na kukosa kasi lakini ikaja kuchangamka mwishoni.
Mchezaji wa timu ya Karabani akirusha mtupo wa adhabu
Mchezaji wa timu ya Adam Juma, Kisoki
Mchezaji wa timu ya Karabani akishusha pumzi
Kibao cha magoli
Adam Juma akaibuka na ushindi wa vikapu 81 kwa 74 dhidi ya timu ya Karabani.
Karabani akikabidhi shilingi milioni moja kwa Adam Juma
Adam Juma akimpoza Karabani baada ya timu yake kushinda
Adam Juma akiongea baada ya timu yake kuibuka na ushindi
Mechi ilisindikizwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali
Rapper Slim Sal akitumbuiza
Rapper akitumbuiza wakati wa mapumziko
Dj Pac akisimamia burudani yote uwanjani hapo
Mastaa kibao walijitokeza kushuhudia mechi hiyo
Diamond Platnumz alikuwepo pia kushuhudia mechi hiyo
Agnes Masogange akiwa na Linex
Aika na Vanessa Mdee
Godzilla
Jan B, Joh Makini, Nisher na Micky
Jux na Izzo B
Marco Chali
Namshalii akiwa na Nahreel
Profesa J alikuwepo kuwaipa support timu ya Adam Juma
Shetta
DeeAndy na Nickson George wa Clouds FM/TV
Godzilla na Salama Jabir
Adam Mchomvu
Diamond Platnumz alikuwepo pia kushow some love
Batu Tale
DJ Choka, Salama Jabir na Godzilla
Warembo kibao walihudhuria
DeeAndy akipima mkono wake kwa mrusho wa pointi mbili
Mrembo akifuatulia mechi kwa makini
Mrembo akijaribu kurusha mpira golini
Mrembo akisalimia na rafiki yake
Mrembo wa Sprite
Msichana akijaribu bahati yake kwa kurusha mtupo wa pointi mbili
Msichana akijaribu kufunga pointi mbili
Warembo wa kizungu wakifuatilia mechi
Warembo wakifurahia mechi
Wasichana wa timu ya Adam Juma
Country Boy, Young Killer na Young Dee washoot video ya wimbo wao ‘Akili za Usiku’
Country Boy, Young Killa na Young Dee wakishoot video yao
Adam na Nisher wakutana
Adam Juma na Nisher waliowahi kutupiana vijembe mwaka jana, walikutana na kuonekana kuweka tofauti zao pembeni huku Nisher akisisitiza kuwa kuna umuhimu wawili hao kufanya collabo kwenye kazi moja ya video.
Picha zingine
Andrew Mahiga
Mtoto anayeishi katika mazingira magumu akiwa na wenzake kushuhudia mchezo huo
Steve Mishe Mishe (Nyama Choma Festival) na Michael Baruti wakiwa na rafiki yao
Wapenzi wa mchezo wa kikapu wakifuatilia kwa makini mchezo
Asha Baraka na Queen Darleen wakimpongeza mchezaji wa timu ya Karabani, Baraka