Michezo
B-Ball Kitaa Presents: The 2 Million Match – Team Karabani vs Team Adam Juma
Karabani na Adam Juma ni waongozaji na watengenezaji maarufu wa video za muziki, matangazazo ya biashara na vitu vingine. Wameamua kuupeleka ushindani wao kwenye uwanja wa kikapu na kuandaa mechi ya kuwania shilingi milioni 2.
Karabani atakuwa na timu yake itakayochuana na timu ya Adam Juma ambapo kila timu itaweka mezani shilingi milioni 1. Mshindi atachukua zote shilingi milioni 2.