Burudani

Baada kumwaga machozi kisa Diamond, Nisha apagawishwa na penzi la Ex-Boy Friend wa Wolper

Msanii wa Filamu Bongo, Nisha kwa sasa ni furaha tele usoni mwake mara baada ya kuingia katika mahusiano na aliyekuwa boy friend wa Jacqueline Wolper, Brown.

Wawili hao wameonekana kuwa karibu zaidi kupitia mitandao ya kijamii na hii baada ya wote wawili mahusiano yao ya awali kuvunjika.

Utakumbuka Nisha alikuwa akidate na kijana ambaye baadaye alikuja kudai kuwa amehamishia penzi lake kwa muimbaji Snura, hata hivyo Snura alikanusha hilo, hivyo hivyo kwa Brown alitoka kuachana na Jacqueline Wolper.

March 12 mwaka huu Nisha aliposti video Instagram akionekana akiilia huku wimbo wa Diamond ‘Sikomi’, ukisikika, video hiyo ilitafsiriwa kuwa mrembo huyo ametendwa na mapenzi kutokana na maudhui ya wimbo huo ila kwa sasa kwa Brown ni kinyume cha hapo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents