Burudani

Baada ya Irene Uwoya, Dogo Janja kuongeza mke wa pili

Msanii wa muziki Bongo, Dogo Janja amefunguka mipango yake ya kuoa mke wa pili.

Dogo Janja ambaye alimuoa Irene Uwoya mwaka jana ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa kuoa mke wa pili hadi wa nne ni moja ya mipango yake na atafanya hivyo kila baada ya miaka 10.

“Inshallah kuongeza wa pili, wa tatu, wa nane hapo ukishakaa vizuri kiuchumi na mwenzako aweze ameridhia,” amesema.

“Hata wanne sio mbaya hapo tunaongelea Mwenyenzi Mugu akitujalia uhai labda baada ya miaka 10 naweza kuongeza wa pili, ikifika miaka 10 tena naongeza, yaani nikifika miaka 50 pale niwe nimekamilisha wanne,” ameongeza.

Soma Pia: Irene Uwoya na Dogo Janja wafunga ndoa

Dogo Janja na Irene Uwoya waliripotiwa kufunga ndoa November 25, 2017, hata hivyo ni vigumu kutaja tarehe kamili kutokana na namna walivyoliweka suala hilo hasa kwa upande wa vyombo vya habari na mitandao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents