Habari
Baada ya kimya kirefu Belle 9 atoa single mpya ‘Wanitaka’ (Audio)
Baada ya kimya kirefu msanii kutoka mji kasoro bahari Belle 9 ameachia single mpya ‘Wanitaka’.
Akiutambulisha wimbo huo muda mfupi uliopita katika XXL ya Clouds FM Belle amesema wimbo huo umetengenezwa na producer aliyetengeneza hit song yake ya mwanzo ‘Sumu ya Penzi’.
“Amefanya Tris, Tris saivi yupo South Africa anasomea sound engineer pia ana direct video, kwasababu ni producer ambaye nimefanya nae kazi akiwa huku kwahiyo yuko kule kanitumia mdundo nikauandikia”. Amesema Belle.
Belle amesema amechelewa kutoa wimbo mpya kutokana na kuwa na tour nyingi pamoja na kuandaa album yake ‘Vitamin Music.
Usikilize hapa
[soundcloud url=”https://api.soundcloud.com/tracks/121969002″ width=”100%” height=”166″ iframe=”true” /]