Muziki
Baada ya misukosuko ya BASATA, Nay wa Mitego aja na wimbo ‘Hakuna Maisha Magumu’ (Video)
Msanii wa muziki wa hip hop, Nay wa Mitego Jumatatu hii ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao 'Hakuna Maisha Magumu'. Rapa huyo hajazoeleka kuja na nyimbo za aina hizo kwani mara nyingi amekuwa akiachia ngoma ambazo zimekuwa zikiikosoa serikali pamoja na kuzungumzia harakakati. Rapa huyo aliitwa Baraza la Sanaa Taifa BASATA zaidi ya mara mbili kuhusiana na wimbo wake uliopita uitwao 'Alisema'.