Baba yake Neymar kataja ofa ya pound milioni 144.4 kwa ajili ya Neymar
Mshambuliaji wa klabu ya FC Barcelona ya Hispania na timu ya taifa wa Brazil Neymar. Kuna stori ambayo imepamba headlines za gazeti la The Sun, ni kuhusu Neymar kuhusishwa kuhitajika na klabu ya Man United ya Uingereza ambayo inatajwa kutenga dau la uhamisho wa kihistoria katika soka, Man Uneted wanatajwa kutenga dau la pound milioni 144.4 kwa ajili ya Neymar.
Hizi stori za Neymar kuhitajika kwa dau la pound milioni 144.4 inadaiwa kutolewa na baba yake mzazi, ambaye amesema kuwa tayari amepokea ofa ya pound milioni 144.4 kutoka kwa vilabu vya Ulaya lakini sio klabu ya Real Madrid, Neymar Sr hakusema jina la klabu ambayo inayomuhitaji Neymar, ila uchunguzi wa The Sun ndo unatajwa kufanikiwa kujua jina la klabu ambayo inasemakana kuwa ni Man United.