BurudaniDiamond Platnumz

Baby Madaha: Diamond ni ‘wahapahapa’ mimi ni international

Baby Madaha amesema kamwe hawezi kucheza ligi moja na Diamond Platnumz. Akiongea na kipindi cha Hot Mix cha EATV Ijumaa hii, muimbaji na muigizaji huyo wa ‘The Gal Bladder’ amesema Diamond ni msanii ‘wahapahapa’ huku yeye akifahamika kimataifa zaidi.

diamondmadaha

Aliongeza kuwa pamoja na kufanya muziki, yeye pia ni muigizaji mzuri wa filamu wakati Diamond ni muimbaji peke yake na hivyo kamwe hawezi kuwa level moja na hitmaker huyo wa Roho Yangu.

Kwa muda sasa, mafahari hao wamekuwa wakirushiana madongo huku Baby akisema Diamond hajui kuimba kulinganisha na msanii kama Ali Kiba.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents