Habari

Baki ‘Mule Mule’ na Vodacom katika msimu huu wa sikukuu za Krismasi na mwaka mpya

Mtandao supa wa simu za mkononi nchini, Vodacom, msimu huu wa sikukuu umeongeza kiwango cha kugawa zawadi kwa wateja wake hadi kufikia shilingi bilioni moja, kupitia Tuzo Points.


Tuzo Points hizo zimekuwa zikitolewa kwa wateja wa VODACOM kila wanapotumia huduma zake mbalimbali, kama vile kuongeza salio, kununua vifurushi na kulipia huduma mbalimbali kwa njia ya M-Pesa.

Kauli mbiu ya Vodacom katika msimu huu wa sikukuu, ni ‘baki mule mule kwenye Vodacom’ ambapo mteja anaweza kupata maelezo zaidi juu ya ofa hii ya msimu wa sikukuu, kwa kupiga namba *150*00#.

Ili kujiongezea nafasi ya kushinda kwa mteja wa Vodacom, pakua M-Pesa App, ongeza muda wa maongezi na kufanya miamala ujikusanyie Tuzo Points nyingi zaidi ambazo unaweza kuzibadilisha na kuzitumia kadrio utakavyo, kutoka muda wa maongezi au kifurushi hadi fedha ya kulipia chochote kwa M-Pesa.

Ndiyo maana Vodacom wanakwambia Baki Mule Mule, huna sababu ya kwenda kule! Yajayo yanafurahisha! Unaweza kutembelea https://vodacom.co.tz/sw/vodacom_points_overview kufahamu zaidi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents