Michezo
Balaa lamkumba Ngassa
Kiungo mshambuliaji wa Azam FC Mrisho Ngassa amepata balaa baada ya kugundulika ana matatizo ya kiafya hivyo kutakiwa kufanyiwa matibabu kabla ya kuanza kwa ligi kuu Tanzania bara Agosti 21 mwaka huu.
Akizungumza na bongo5 jijini Dakatri mkuu wa Azam Nassor Idrisa alisema kuwa Ngasa amegundulika na tatizo la misuli ingawa kwa sasa linaendelea kushughulikiwa.
Pamoja na hilo kikosi kizima kinatarajiwa kuenda kukifanyia uchunguzi wa afya ili kujua kama kuna mchezaji mwenye matatizo na aweze kutibiwa.
“Kila kitu kinaenda sawa jumamosi tunatarajia kwenda kupata matibabu ili kuandaa timu yetu kabla ya kuanza kwa ligi kuu” aisema Nassor.