Bamboo: Diamond Platnumz sio ‘type’ ya Victoria Kimani
Kaka yake na muimbaji wa Kenya, Victoria Kimani, Bamboo amesema haoni tatizo dada yake huyo kuwa na mwanaume japo amekanusha vikali tetesi zozote za kama ana uhusiano na Diamond Platnumz.
Bamboo ameuambia mtandao wa rapnairobi kuwa Diamond si aina ya wanaume wa Victoria. “I doubt that, Diamond is not her type, there was still one with Wanyama. If she’s dating a guy anaeza akidecide. She’s a grown woman. She has worked hard, people don’t know that she also featured on Nairobiz album, that’s like K-south second album so ametoka far,” alisema.
Hivi karibuni Diamond aliiambia Bongo5 kuwa Victoria ni rafiki yake tu. “Victoria mwanangu tu, rafiki yangu, anaappreciate kazi zangu na siku moja aje kufanya kazi na mimi. Ni kazi tu na sio kwasababu mimi na mwanaume na yeye ni mwanamke, na ukimwangalia ni mwanamke mzuri so wanajua tu naweza kumdate lakini sio kila siku simba anakuwa na njaa sometimes hata yeye anafunga pia.”