Burudani
Banky W na Adesua Etomi wamalizana kiserikali
Msanii wa Nigeria, Banky Wellington maarufu kma Banky W na Adesua Etomi rasmi ni mke na mume kisheria.
Wawili hao wametambulika rasmi na serikali kuwa ni wanandoa baada ya leo (Jumatatu) kusaini hati za kisheria katika sherehe binafsi.
Siku ya jana wawili hao walifunga ndoa yao ya kimila mjini Lagos.