Michezo
Barcelona watawala kikosi bora cha wiki, Man United, Chelsea na Bayern majanga matupu
Shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA) limetangaza kikosi bora cha wiki hii (Machi 13-14, 2018) kwenye michuano ya klabu bingwa barani Ulaya ambapo klabu mbili kutoka Uingereza za Chelsea na Manchester United na moja kutoka Ujerumani zimefanikiwa kutoa mchezaji mmoja mmoja
Kwenye kikosi hicho Klabu ya Barcelona ndio klabu iliyotoa wachezaji wengi (4) ikifuatiwa na Roma wachezaji watatu na Bestikas mchezaji mmoja.
Kwenye kikosi hicho ambacho wanaangalia mchango wa mchezaji mmoja mmoja kwenye nafasi yake, klabu ya Bayern imefanikiwa kuingiza mchezaji mmoja ingawaje jana Machi 14, 2018 wameichabanga Beskitas goli 3-1 .