Burudani
Barnaba aanzisha bendi yake ‘Barnaba Classic’
Barnaba ameanzisha bendi yake mwenyewe.
Muimbaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa bendi yake ilikuwepo lakini sasa itakuwa na vifaa vya kisasa.
“Nina bendi toka muda mrefu ila sasa hivi ndo naifanya official. Naanza kunua vifaa vyangu vya muziki au kama akitokea mtu akaninunulia sio mbaya pi,” amesema.
“Bendi itakuwa ni bendi tofauti zingine zote unazozijua. Mimi sitapiga kama wengine kwenye maukumbi, sitafanya hivyo. Bendi yangu itakuwa ni kwaajili ya shughuli maalum, kwenye sherehe kubwa, matukio yoyote makubwa itakuwa inafanya,” ameongeza.