Burudani

Barnaba Azidi Kukumbwa Na Gubu, Balaa Lingine Lamkumba

Barnaba Akitabasamu na gitaa lake lililoibiwa.

Msanii Barnaba Elias ameendelea kuandamwa na mfululizo wa mikosi, baada ya wikiendi iliyopita kuibiwa gitaa lake ambalo alipewa na Mke wa Rais wa Marekani aliyopita Mama Laura Bush. Barnaba alielezea kusikitishwa na tukio hilo ambapo anasema liliibwa maeneo ya Leaders nje ya ofisi za THT ambapo ndipo makao makuu ya kituo chao cha kazi.

Akiongea na Bongo5 Barnaba alisema, baada ya kuingia katika ofisi za THT siku ya jumamosi, majira ya saa kumi na mbili na kufanya mambo yake, alishangaa kutolikuta gitaa lake hilo alilopewa kama prize Asset na Laura Bush, Mke wa Rais aliyepita na alichanganyikiwa kidogo kwa namna lilivyotoweka.

“Ninavyokwambia nilifunga milango yote lakini hawa jamaa wametumia mbinu kali maana hakuna mtu aliyeshituka. Barnaba anasema bado juhudi za kulitafuta gitaa hilo zinaendelea na anasema atashukuru kama atapata mtu atakayemsaidia kwa taarifa ili kulipata gitaa hilo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents