Burudani
BASATA waishushia rungu kampuni ya U-Miss (Video)
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeifungia kampuni iliyoandaa Shindano la Miss Tanzania Mbeya kwa kufanya shindano bila kufuata taratibu za BASATA zilizowekwa kisheria. Akizungumza na Bongo5 Jumatano hii, Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Godfey Mngereza amesema kampuni hiyo imefungiwa kwa mujibu wa sheria baada ya kukiuka taratibu za BASATA.