Burudani

BASATA yakanusha kuufungulia wimbo wa ‘Mwanza’, latoa tamko kali kwa Rayvanny

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetoa tamko kwa umma, vyombo vya habari na jamii kwa ujumla kuwa halijaufungulia wimbo wa ‘Mwanza’, uliyoimbwa na msanii wa WCB, Rayvanny kwa kushirikiana na DiamondPlatnumz.

 

BASATA imesisitiza kuwa daima limekuwa likifanya kazi zake kwa weledi mkubwa na kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo iliyopo. Hivyo taarifa za kufunguliwa wimbo huo sio za kweli ni za kizushi, aidha jamii inatakiwa kuzipuuza taarifa hizo ambazo hazina chanzo maalum.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents