Michezo
Beckham anatamani kubaki Italy kimoja!!
Mchezaji David Beckham wa LA Galaxy amesema ataendelea kubaki AC Milan mpaka Mzunguko wa ligi hii ya Italy utakapomalizika mwezi May 31 mwaka huu.
Akiongea na gazeti moja la kila siku la Italy David Bekham amesema kwamba pia atajiunga na timu yake ya Taifa ya England kwa ajili ya michezo miwili ya awali ya Kombe la dunia kabla ya kujiunga tena na timu yake ya LA Galaxy mwezi July.
Aidha Bekham huku akiongea akicheka alijibu swali la mwandishi huyo alisema kuwa anatamani kuondoka LA Galaxy na kubakia Italy kimoja.