Michezo
Beckham aongeza tattoo kuukumbuka mwaka 1999 akiwa Manchester United
Mchezaji wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya England, David Beckham kupitia katika akaunti yake ya Instagram ameonesha Tattoo mpya.
Kujichora kwa Beckham tattoo hiyo ina maana ya kumbukumbu ya msimu wa 1998-99 ambao Manchester United ilishinda makombe matatu, kombe ‘Treble’ la FA na ligi ya mabigwa Ulaya pamoja na la ligi kuu ya England. Pia Beckham amechora tattoo ya namba 99 katika kidole chake cha mkono wa kushoto.
Mchezaji huyo wa zamani ameandika, Beckham, ’99 was a good year for me.’