Michezo

Bei ya jezi mpya ya Ronaldo ‘Juventus’ ni mshahara wa mwalimu Tanzania

Imekuwa ni wiki yenye furaha kwa Mreno, Cristiano Ronaldo baada ya kuvuta mkwanja mrefu  kutoka klabu ya Juventus wakati mashabiki wa vibibi hao wa Turin wakimiminika kununua jezi za staa huyo.

Rasmi Cristiano Ronaldo ajiunga na Juventus ya Italia

Jezi halisi ya Ronaldo ambayo imetengenezwa na klabu ya Juventus ambazo ni za mechi za nyumbani zinagharimu kiasi cha dola 144.95 ambayo ni sawa na Tsh 329715.16.

Jezi hiyo hiyo ya nyumbani kwa upande wa wanawake inagharimu kiasi cha dola 94.95 ambayo ni sawa na Tsh 215977.78

Jezi hiyo hiyo ya nyumbani ya Ronaldo kopi yake ambayo siyo origino inauzwa kwa kiasi cha dola 104.95 sawa na Tsh 238687.62

Wakati kwa watoto jezi hiyo ya nyumani unaweza kuinunua kwa dola 79.95 ambayo ni sawa na Tsh 181,848.64.

Wakati mshahara wa mwalimu hapa nchini kima cha chini ni sawa na Tsh 331000 kwa mwezi.

 

 

 

Ronaldo mwenye umri wa miaka 33, ameingia kandarasi ya pauni milioni 105 kutua Juventus siku ya Jumanne akitokea Real Madrid.

 

Ronaldo alikutana na rais wa timu ya Juventus, Andrea Agnelli mchana wa siku ya Jumanne kwenye hoteli huko Greece ambapo alikuwa mapumzikoni na mpenzi wake pamoja na familia kabla ya kukubali dili hilo la miaka minne ambalo atavuna kiasi cha pauni 500,000 kwa wiki.

Hapo jana siku ya Alhamisi nyota huyo ameonekana akifurahia maisha na familia yake akiwa sambamba na marafiki zake akiposti picha kwenye instagram inayo muonyesha akipata chakula cha usiku.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents