Habari
Beka atarajia kusaini mkataba mnono na Sky Light Band (Audio)
Msanii wa muziki Beka Ibrozama amesema yupo kwenye mazungumzo ya makubaliano ya mkataba wa kujiunga na Sky Light Band yenye makazi yake jijini Dar es salaam.
Beka akifanya show siku ya Eid akiwa na Skylight Band
Beka ambaye ameachia wimbo mpya, Bijou, amesema ingawa tayari ameanza kufanya kazi na Band hiyo yenye wapenzi wengi jijini Dar es salaam bado hajasaini mkataba kutokana na mabosi wa Band hiyo kuwa safarini.
“Wamejua umuhimu wangu na wameona mimi endapo nikiwa Skylight labda kuna kitu kitatokea, mimi kutoka moyoni naipenda Skylight kwasababu ni band ambayo nahisi inafanya kitu kikubwa sana hapa Tanzania, sijawai kuona,” alisema Beka.
[soundcloud url=”http://api.soundcloud.com/tracks/105367194″ params=”” width=” 100%” height=”166″ iframe=”true” /]