Msanii Belle 9 anayetokea Morogoro lakini siku ya alhamisi alifanya video yake ya tatu kwa jina ‘Nilipe Nisepe’.
Akizungumza na Bongo5 Belle 9 alisema Video hiyo ni mfululizo wa Video ambazo alipanga kufanya katika kasi ya kutengeneza albamu yake ya pili ambayo anaiita ya kwake binafsi ambapo amefanya nyimbo kibao na producer wake Mona wa Masanjua Records ya Mwenge jijini Dar-Es-Salaam.
Aidha msanii Belle 9 alisema katika siku si nyingi atadondosha video ya wimbo ambao ameshirikiana na Mr Blue so mafans wakae mkao wa kula.