Burudani
Ben Pol: Nipo tayari kurudi tena shule
Muimbaji wa ‘Sophia’ Ben Pol amedai kuwa kwa sasa yupo tayari kurejea shule.
Ben aliwahi kuwa mwanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha, IFM lakini hata hivyo hakuweza kumaliza masomo.
Akiongea kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa hii, msanii huyo amedai kuwa hakuacha shule kama watu wanavyodhani bali aliahirisha mwaka kwa matarajio ya kuja kurejea tena baadaye.
Amedai kuwa hivi karibuni amekuwa akiangalia mbadala wa kusoma Open University. Ben anadai anaona sasa anaweza kuendelea tena na masomo.