Burudani
Benjamini kuwakusanya 20% na Baghadad
mwanamuziki Benjamini wa Mambo jambo amesema wimbo wake wa My Friend anataka kuutoa upya huku akimshirikisha mkali wa Bongo Fleva aliyejizolea Tuzo tano, Abas Kinzasa maarufu kama 20% kutoka FAM Boys na mtu mnene toka Maxicana Lacavera Baghdad, kwa pamoja wanaungana ilikuikamilisha wimbo huo.
Benjamini anasema kuufanyia ‘Rhymix’ wimbo huo, ni kuonyesha mapenzi ya kweli kwa mashabiki wake, ambao anawapenda sana kwakuwa wao ndiyo waliomfanya awe juu, na hata wimbo huo kuingia katika Kili Music Award.
Anasema anawapenda sana wapenzi wake, na ndiyo maana akaamua kuchanganya radha iliatoe kitu cha uhakika.