Benki ya NMB yaja na huduma tatu za kidijitali, sasa utafungua akaunti ya benki kupitia simu ya mkononi
Katika kukabiliana na ushindani na kasi ya mabadiliko ya teknolojia nchini, Benki ya NMB Plc imeingiza sokoni huduma tatu kwa mpigo za kibenki kidijitali ikiwemo ya kufungua akaunti ya benki ndani ya dakika tatu kwa kutumia simu ya mkononi.
Huduma hizo tatu zilizozinduliwa ni uwezo wa mwananchi kufungua akaunti kupitia simu yake ya mkononi, App yenye huduma zote ambazo mteja anaweza kufanya mwenyewe badala ya kwenda kwenye tawi na huduma ya Scan to Pay huduma ya kufanya malipo kwa kutumia QR code. App ya NMB KLiK inapatikana katika Playstore https://goo.gl/Fr9fZf na kupitia AppStore https://goo.gl/wQXZV6
https://youtu.be/wrwNLBmn8a0
Mkuu wa Idara ya Ubunifu wa benki hiyo, Josina Njambi amesema huduma tatu zilizozinduliwa zinajumuisha namna mpya ya kujiunga na benki (accessebility), namna mpya inayomwezesha mteja kutumia benki yake kikamilifu kidijitali na huduma ya tatu inalenga zaidi kujenga jamii isiyotegemea pesa za mifukoni (Cashless society).
Njambi amesema huduma hizo zitakuwa zinafuata nguzo tano ambazo ni kufikiwa kwa urahisi popote ulipo Tanzania, kurahisisha huduma za benki hiyo kwa wateja wake, huduma za haraka, iliyosalama na huduma kutokana na mahitaji ya wateja.
Kwa wanaotumia simu janja maarufu kama smartphone, huduma hizo zinapatikana katika programu ya simu iitwayo NMB Klik wakati wale wenye simu za kawaida zilizopewa jina la utani za “Vitochi” watatumia ujumbe mfupi wa maneno (Shortcode Sms).
Katika mabadiliko hayo, Njambi amesema wateja wa benki hiyo wanapofungua akaunti hawatalazimika kutumia “fomu za makaratasi, kulipia gharama za kufungulia, masharti ya kuchosha na wala hawatahitajika kufika katika tawi la benki”.
“Mtu anayetaka kufungua akaunti atahitajika kuwa na moja ya vitambulisho vya aina tano ambavyo ni leseni ya gari, kitambulisho cha taifa, kitambulisho cha kupigia kura, pasi ya kusafiri na kitambulisho cha Mzanzibari mkazi mteja wa benki ya NMB ataweza kutumia kitambulisho kimoja wapo kufungulia akaunti kupitia simu kwa kuboonyeza *150*66# kujiunga.
Uzinduzi huo uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt umehudhuriwa na Naibu Gavana Usimamizi wa Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dk. Benard Kibese ambaye alisema kwamba ubunifu huo utarahisha Watanzania wengi kufungua akaunti za benki hiyo kupitia simu zao za mikononi na kwamba hivi sasa watumiaji wa simu za mkononi ni wengi na hivyo huduma hiyo ya NMB imekuja wakati sahihi.
βTunaipongeza NMB kwa ubunifu huu ambao wamekuja nao wa kuhakikisha wanatumia teknolojia iliyopo kuanzisha huduma za kufungua akaunti kupitia simu ya mkononi na kizuri zaidi hata wenye simu za tochi bado wanaweza kufungua akaunti kupitia huduma hiyo,β amesema Dk. Kibese.
Huduma hiyo imepokelewa vizuri na watumiaji wa mtandao wa Twitter ambao wamesema kwamba uzinduzi huo ni muhimu sana hususani katika mchakato wa kuipeleka Tanzania katika Uchumi wa kati.
@NMBTanzania hii app yenu nimeirate 4.9 out of 5. Ipo designed proffesionally
Great job#changeTanzania
I am banking at my comfort with NMB KLiK app. Download here https://t.co/PWaIFLiPrg— @mfukunyuzi (@libeberu) August 15, 2018
@NMBTanzania Hii #NMBkLik niπ₯π₯π₯ππSafi sana!
— Musti (@z_yIIV) August 15, 2018
Habari ya mjini ni NMB Klik na@NMBTanzania
You deserve. pic.twitter.com/7STrcun597— Kasyeto Pandora (@kasyeto) August 15, 2018
The new NMB KLiK App is revolutionizing the mobile banking in Tanzania like never before π₯π₯π₯π₯ congrats @NMBTanzania for major milestone
— Julius J. Mbungo II (@007juelz) August 15, 2018
https://twitter.com/PatNanyaro/status/1029317002589024258
Waambie nishafungua akaunti tayari,kule kwetu Simiyu sipati shida tenaaa mwendo wa *150*66# (Hapa nimefanya promo free) pic.twitter.com/G371f92Nyq
— Justine Limbe Jr (@16Limbe) August 14, 2018
Mwanzo wa safari mpaka sasa #NMBJourney pic.twitter.com/tWP91YbgXo
— Uncle Fafi (@Tanganyikan) August 14, 2018
Good two days for #Innovators in #Tanzania … 1st @NMBTanzania ππ launched KLiK and now @FSDTanzania launches #FinSightsLab ππ #FinancialInclusion pic.twitter.com/OTvIIENZqN
— Blandina Kilama (@BBuganzi) August 15, 2018