Burudani
Beyonce anawakaribisha mapacha wake kwa style hii
Ikiwa zimebaki wiki mbili kwa mujibu wa baba yake mzazi wa mwanamuziki Beyonce,Mathew Knowles kupokea wajukuu wapya, Familia ya Carter yafanya sherehe kuwakaribisha mapacha hao.
Katika sherehe hiyo iliyofanyika siku ya jumammosi na kupewa jina la”Carter Push Party” yenye lengo ya kujiandaa na kuwakaribisha unborn wao wapya, ilihudhuriwa na watu wachache maarufu wakiwemo kundi la Destiny’s Child -Michelle Williams na Kelly Rowland pamoja na mama yake mzazi Beyonce ,Lala Anthony na Serena Williams.
Shughuli mzima iliongozwa na Qeen B mwenyewe huku akiwa amevalia kiafrika, na baadhi ya sehemu la tumbo hilo likiwa limechorwa tattoos. Sherehe hiyo ya The Carter push party ama baby shower ilifanyika nyumbani kwake.
Na Laila Sued