Habari

Bi Nasma Khamisi Kidogo, kumbe bado wamo?

Nasma Khamis KidogoMsanii mkongwe katika muziki wa mwambao nchini Tanzania yaani taarabu Bi Nasma Khamisi Kidogo hivi karibuni ametoka tena na albam yake mpya itakayokwenda kwa jina la ‘dawa ya deni’

Nasma Khamis Kidogo


Msanii mkongwe katika muziki wa mwambao nchini Tanzania yaani taarabu Bi Nasma Khamisi Kidogo hivi karibuni ametoka tena na albam yake mpya itakayokwenda kwa jina la ‘dawa ya deni’ na pia ameachia ngoma zake mbili ambazo zinatarajiwa kuwa ni tishio katika muziki huo unaoonekana kupanda chati kila kukicha.


Albam ina jumla ya nyimbo sita na imerekodiwa katika studio za sound crafters zilizopo maeneo ya Chang’ombe na hii ikiwa ni albam ya pili kutoka kwa msanii akiwa kama msanii wa kujitegemea.


‘nazijua nizipendazo’ ndio jina la albam iliyopita ya msanii huyu mkongwe, ambapo alitamba na vibao kama ‘mahaba ya dhati na tunapendana kwa dhati’ ambazo mpaka leo bado zinafunika ile mbaya katika medani ya muziki wa taarabu hapa jijini.


“japo nazeeka lakini naamini mimi ni msanii na naipenda sana kazi yangu hivyo sichoki kabisa kufikiria mbinu mpya za kuifanya sanaa yangu isizeeke, ndio maana hata katika albam yangu hii mpya nimejaribu kuja tofauti na kwa kufanya nyimbo zenye mahadhi ya zouk, Rn’B, pia kuna nyimbo nimerap.


Mwanamama huyu amewahi kutamba sana na vibao vyake kama vile ‘mambo iko huku’ alipokuwa katika kundi lililowahi kujinyakuia umaarufu hapa jiji la Muungano culture troup.


Sikiliza “Sabal Kheri”
{play}nasma_khamis_kidogo_sabal_kheri.mp3{/play}

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents