Burudani

Big Brother Africa: Nando wa Tanzania kwa mara ya kwanza hatarini kutoka wiki hii, kura yako inahitajika kumuokoa

Ni wiki tatu zimepita tukishuhudia Eviction shows tatu zilizowapa tiketi za kurudi makwao washiriki 6 mpaka sasa, na tumeshuhudia mshiriki wetu Feza Kessy akiponea kwenye tundu la sindano baada ya kura za wa Tanzania na wa Afrika kumuokoa, sasa ni zamu ya Nando ambaye yuko hatarini wiki hii.

AmmyNando2

Big Brother jana ametaja majina ya washiriki 7 ambao wako hatarini kutoka wiki hii na kati yao yupo kijana mpole, mtanashati, ‘handsome’ Nando anaeiwakilisha Tanzania, ikiwa ndio mara yake ya kwanza kupendekezwa .

Washiriki wengine walipigiwa kura nyingi kutoka wiki hii ni love birds Bolt na Betty, ambao hii si mara yao ya kwanza kupendekezwa baada ya kuponea chupuchupu kwa mara kadhaa.

Kenya wiki hii iko salama kwa mshiriki wao mmoja aliyesalia Annabel, japo kuwa alipendekezwa kutoka wiki hii lakini kilichomuokoa ni yeye kuwa mkuu wa nyumba ya Diamond, hivyo amepata favor ya kujiokoa mwenyewe na nafasi yake akampendekeza Motamma wa Botswana.

Kwa ujumla walioingia wiki hii ni Nando wa Tanzania, Natasha wa Malawi, Oneal wa Botswana, Motamma wa Botswana, Betty wa Ethiopia, Bolt wa Sierra Leon na Elikem wa Ghana.

Tanzania bado ina nafasi nzuri sababu washiriki wote wawili Nando na Feza wapo mjengoni na ndio maana unakila sababu ya kumpigia kura mara nyingi uwezavyo Nando ili aweze kubaki wiki hii. Washiriki wawili kati ya saba waliopendekezwa watapita kwenye mlango wa ‘EXIT’ mjengoni hapo Jumapili hii (June 23) wakati wa Eviction Show.

Ladies and Gentlemen please VOTE, VOTE, VOTE, VOTE for NANDO!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents