Habari
Bill Gates atua nchini ‘kimya kimya’ na kutembelea miradi ya afya Tanga
Mfanyabiashara maarufu na tajiri namba moja Duniani, Bill Gates yupo nchini Tanzania kutembelea miradi mbalimbali ya afya ikiwemo mradi wa matumizi ya dawa za matende na mabusha.
Bill Gates leo mapema alikuwa mkoani Tanga na kutembelea baadhi ya vituo vya afya mkoani humo na kuonana na baadhi ya viongozi wanaosimamia miradi hiyo.
Hata hivyo kuna taarifa kuwa tayari Bilionea huyo ameshafika jijini Dar es salaam .