Habari
Binti mdogo muuza viatu vya mtumba aliyekuza mtaji kutoka tsh 40000 hadi tsh milioni 5 (Video)
Takwimu zinaonyesha kwamba idadi kubwa ya wajasiriamali nchini Tanzania ni wanawake. Bongo5 wiki katika Kona ya Mjasiriamali Kijana imekutana na binti mwenye miaka 22 ambaye anajighulisha na biashara ya kuuza viatu vya mtumba. Binti huyo ambaye anatumia brand ya Mamu Knows alianza biashara hiyo kwa mtaji wa tsh 40000 na mpaka sasa tayari ana mataji wa tsh milioni 5 huku akiwa na maduka mawili pamoja na wafanya kazi watatu.