Burudani
Birdman atawapoteza Drake na Nicki Minaj kwa uzembe wake – Lil Wayne
Lil Wayne amedaiwa kumtupia lawama bosi wake Birdman na Cash Money kuwa ni mzembe kiasi ambacho anakaribia kuwapoteza, Nicki Minaj na Drake.
Kwa mujibu wa ripoti ya TMZ, Lil Wayne amewasilisha mashtaka mengine akitaka kumuondoa Birdman kutoka Young Money, label iliyowasainisha Nicki na Drake.
Wayne anadai kuwa Birdman na Cash Money wameshindwa kuindesha kampuni. Amesema uongozi ni mbaya kiasi ambacho Nicki na Drake wanaweza kuondoka.