Burudani

Black Panther yazidi kutikisa dunia, yaingiza dola bilioni 1.182

Filamu ya ‘Black Panther’ imezidi kufanya vizuri katika mauzo yake duniani.

Filamu hiyo imetajwa kuingiza kiasi cha dola milioni 605.4 kwa Marekani ndani ya mwezi mmoja tangu ilipotoka February 16 ya mwaka huu, pia imeingiza kiasi cha dola bilioni 1.182.5 duniani kote.

Kutokana na kiasi hicho kilichoingiza filamu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya Marvel Studios, imevunja rekodi zilizowahi kuwekwa na filamu kibao kwenye box office.

Black Panther ambayo imeongozwa na Ryan Coogler, ilitumia bajeti ya kiasi cha dola milioni 200–210 katika kuitengeneza.

Black Panther imewakutanisha waigizaji kama Chadwick Boseman ambaye ndio staa wa filamu hiyo, Lupita Nyong’o, Michael B. Jordan, Danai Gurira, John Kani na Connie Chiume.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents