Burudani
Bob Junior awapongeza watayarishaji wa muziki wa Bongo
Muimbaji na mtayarishaji wa muziki, Bob Junior amesema watayarishaji wa muziki wa sasa wamefanya kazi kubwa kuupeleka muziki mbele kuliko wa zamani.
Bob Junior amesema watayarishaji wa sasa wamezifanya nyimbo nyingi za Tanzania kuweza kupenya kwenye tuzo mbalimbali.
“Sasa hivi production ipo vizuri sana. Tunaendelea kwa sababu tumekuwa nominated katika tuzo mbalimbali kubwa Afrika,” ameiambia Bongo5.
“Kwahiyo ni hatua. Zamani ilikuwa haipo, sasa hivi ukiangalia Kenya, Uganda na Tanzania tunakuwa nominated kwenye tuzo za afrika kabisa kwahiyo ni moja ya hatua nzuri katika muziki wetu na watayarishaji wetu.”