Bob Junior ni zaidi ya msanii
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Bob Junior, Raisi wa Masharobaro au Mr Chocolate Flavour , amesema hivi sasa msaada hatojali kuinua vipaji vipya kwani anajua bado unahitajika msaada wake kwa wasanii wachanga, ingawa watu wengi wamekuwa wakijifanya kama hawauoni.
Mr Chocolate anasema anajivunia sana kipaji alichonacho kwani anakitumia vizuri na watu wanakiona na ndiyo maana wanamuunga mkono kwa kazi zake kama kuibua vipaji vipya. anasema yeye ni zaidi ya msanii kwakuwa anaimba, anawatungia watu nyimbo, kwakuwa hadi sasa anatungia watu na kuwatengenezea biti kwa wale wanaohitaji.
Bob Junior zaidi ya kutengeneza biti na kuibua vipaji vya wasanii wachanga, pia amekuwa mtangazaji katika kipindi cha Bongo Star Search Second Chance 2011, kinachoendelea ITV, .
Amesema yeye hawafuatilii watu ambao watamdhihaki kwa utashi wao, kwakuwa msaada wake unaonekena kwa wale wanaohitaji, ingawa inahitaji moyo wa mtu kushukuru.
Raisi huyo wa Masharobaro amesema hivi sasa ametoa wimbo wake mpya unaitwa Na nini, ambao unafanya vizuri kwenye stesheni mbalimbali za radio baada ya ule wa Muogo, Kiazi
{hwdvideoshare}id=1594|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}