Burudani
Bobby Brown, familia yakusanyika kumuona Bobbi Kristina kwa mara ya mwisho: ripoti
Kuna taarifa kuwa Bobby Brown na familia imekusanyika pamoja kujiandaa kwa habari mbaya ya kumpoteza mtoto wa Whitney Houston, Bobbi Kristina Brown.
Bobbi, 21, bado amewekewa mashine ya kumsaidia kuishi baada ya kukutwa bafuni akiwa hajitambui. Ubongo wake umedaiwa kufa.
Madaktari wamewaambia ndugu zake kuwa hakuna wanachoweza kukifanya kunusuru maisha ya msichana huyo, People.com imesema.
“Kila mmoja anakuja hospitali kumuaga,” mwafamilia mmoja ameliambia jarida hilo. Hadi sasa anayesubiriwa kuamua kutolewa kwa mashine hiyo ni Bobby Brown, baba wa mtoto huyo.
“Bobby amekuwa akilia bila kunyamaza tangu jana,” mtu huyo aliliambia jarida la People. “Tunahuzunika.”