Bobi Wine akamatwa na jeshi la polisi Uganda, waandishi wa habari na wananchi warushwa kichura
Msanii wa muziki na Mbunge wa upinzani nchini Uganda, Bobi Wine amekamatwa tena na jeshi la polisi nchini humo leo mapema baada ya kuwasili Uwanja wa ndege mjini Entebbe akitokea Marekani alikokuwa anatibiwa.
Bado hakuna taarifa rasmi ya jeshi la polisi juu ya kukamatwa kwa Bobi Wine, lakini tayari mamia ya watu wakiwemo waandishi wa habari waliojitokeza kumpokea Bobi Wine mjini Entebbe.
UPDATE: Bobi Wine has been Arrested on touching down at the Entebbe Airport. Museveni didn’t disappoint with primitive energy. #BobiWineReturns #BobiWineHomecoming pic.twitter.com/LgV1JIKOE6
— Kenya West (@KinyanBoy) September 20, 2018
Jana jeshi la polisi nchini humo, lilitangaza kuwa hakuna mtu atakayeruhusiwa kumpokea Bobi Wine ndani au nje ya Uwanja wa ndege isipokuwa familia yake tu.
Tayari watu wanne ndugu zake na Bobi Wine wamekamatwa mchana wa leo huku, mamia ya wananchi waliokaidi amri ya jeshi wakivurumushwa na maji ya washa washa.
Heavy deployment as seen along Entebbe road and neighbouring areas ahead of Bobi Wine's return this afternoon #NTVNews #BobiWineReturns https://t.co/MlY6BfNcKl pic.twitter.com/zQhliFdDA3
— NTV UGANDA (@ntvuganda) September 20, 2018