Siasa

Bobi Wine: kufungwa kwa Intaneti kulivuruga uchaguzi

Bobi Wine amewaambia waandishi wa habari kuwa anaamini intaneti na mitandao ya kijamii vilifungwa ili kuvuruga mchakato wa uhesabuji kura.

Mgombea huyo wa upinzani amedai kuwa kulikuwa na wizi.

Mawakala wake pamoja na wawaikilishi wameendelea kukamatwa.

Lakini mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Simon Byabakama, amesema kuwa Bobi Wine ana jukumu la kutoa ushahidi kwamba kuna wizi.

Amesema kuwa wagombea walikuwa na mawakala ambao walishuhudia kuhesabiwa kwa kura katika vituo vya kukusanya na kuhesabu kura.

Ni vituo viwili tu vya upigaji kura vilivyoripoti dosari na shughuli ya kupiga kura ikasitishwa katika vituo hivyo.

Katika kituo kimoja cha kupigia kura, mtu mmoja alitoroka na sanduku la kura.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents