Bondia Cheka kuzichapa Uingereza
Mwandondi mashuhuri nchini Tanzania Fransis Cheka yupo nchini Uingereza
kwaajili ya pambano lake litakalofanyika Manchester Evening News
Areana, jijini Manchester, Uingerza
Mwandondi mashuhuri nchini Tanzania Francis Cheka yupo nchini Uingereza kwaajili ya pambano lake litakalofanyika Manchester Evening News Areana, jijini Manchester, Uingerza.
Bw. Cheka atambambana na Mathew Macklin tarehe 06 mwezi wa 08 kabla ya pambano la Amir Khan.
Mpaka hivi sasa Bw.Cheka ameshapigana mapambano 26 kati ya hayo amepoteza 5 ametoka sare 1 ameshinda 15 kwa knockout na mapambano 5 ameshinda kwa point.
Bw.Cheka amezaliwa Tanga tarehe 15 mwezi wa 4 mwaka 1982, amepata elimu yake ya msingi Kinondoni,jijini Dar Es Salaam. Bw.Cheka alianza kupigana ngumi za ridhaa mwaka 1999 na mwaka 2001 alianza kupigana ngumi za kulipwa.