Bongo Fleva wawalaza Bongo Movie
Siku ya Jumamosi jioni, kulikuwa na mtanange wa kukata na shoka kati ya timu ya mpira wa miguu ya Bongo Fleva fC, na Timu ya Bongo Movie Fc, katika mechi ya Hisani ya kukusanya fedha za kuwasaidia wahanga wa maathiriko ya Mabomu Gongo la Mboto.
Katika mtanange huo, Bongo Fleva Fc iliibuka kwa ushindi wa bao mbili kwa zero, na yote hayo yalifungwa na H. baba ambaye alizitikisa kisawasawa nyavu ya wapinzani wao.
Mgeni rasmi alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa na mbunge wa Kinondoni Idd Azzan, huku wakishirikisha na wananchi ambao walijaa kwa wingi ili kuja kupata burudani, pia kuchangia kiasi walichonacho kwa waathirika hao.
Timu zote mbili zikiingia uwanjani, kwa kuanza mtanange mzima.
Timu ya Bongo Movie Fc, ikiwa imejipanga katika picha ya pamoja kwaajili ya kupata kumbukumbu.
Mgeni rasmi Jerry Slaa akimsalimia Yusuph Mlela, wakati wakuanza kwa mechi hiyo.
Kipa wa Bongo Fleva akimtambulisha mgeni rasmi Jerry Slaa kwa kocha wake, Prof Jay
Goli la pili alilofunga H. baba hapa likiingia nyavuni.
Mikwara ya Jb na Masanja kwa kuzunguka uwanja, hatmaye wakawa hoi na kuanza kuanguka kiwanjani.
Kanumba akiwa haamini kama kweli amekosa kucheza mechi hata kidogo, ingawa alimbembeleza refa, lakini aliambiwa ‘Sub’ imeisha na haiwezekanai kuingiza tena.
Mgeni rasmi akiwa anasubiri timu ya kuipa kombe.
H.baba akieleza jinsi gani alivyoweza kuliza Bongo Movie, ingawa yeye mwenyewe anaimba nakuigiza.
Marefa walioendesha menchi nzima wakiwa katika picha ya pamoja, walichezesha mpira kwa amani na bila ya upendeleo wakijua kabisa kama hii ni burudani tu.