Bongo Movie C.P.U kurushwa TZ Movie Theatre
Katika utofauti wa namna tulivozoea filamu za Bongo, C.P.U, movie ambayo imekamuliwa na mayoungster kiaina kwenye industry, itaanza kuonyeshwa katika theatre za mubvi Mlimani city hivi karibuni.
C.P.U imeamsha hisia za watu wengi walio kwenye tasnia ya filamu kana kwamba inaweza ikafunika sinema zote tumeshawahi ona kwa ubora kwa story pamoja na ufanisi wa kurekodi. Director wa filamu hii ni kijana ambaye amepata umaarufu fasta punde tu aliporudi kutoka Marekani na kuingia kuanza kurekodi music videos za baadhi za wasanii akiwemo Alikiba na hivi sasa Movies hapa Bongo.
Team Bongo5 imefanikiwa kushuhudia trailler ya Movie hii na kukubali sana jinsi inavyoonyesha kumaanisha kuleta ubora na utofauti kwenye sanaa ya filamu.
Big Up team nzima ya C.P.U