Michezo
Brazil2014: Tweet ya shirika la ndege la Uholanzi, KLM baada ya Mexico kuondolewa yazua hasira
Shirika la ndege la Uholanzi la KLM limepoteza wateja wake wengi wa Mexico baada ya kutweet picha ya kuwatania Wamexico waliotolewa jana kwenye kombe la dunia na Uholanzi.
Dakika chache baada ya Uholanzi kushinda 2-1 dhidi ya Mexico, shirika hilo lilipost picha ya alama ya ‘departure’ ya uwanja wa ndege na kuandika: ‘Adios Amigos #NEDMEX’.
Alama hiyo ilikuwa na nembo ya mtu mwenye mustachi akiwa amevaa kofia ya sombrero, na hivyo kufanya ionekana ya ubaguzi. Post hiyo iligeuka kuwa maarufu kiasi cha muigizaji maarufu wa Mexico Gael Garcia kuandika post kwenye Twitter kuwa hatopanda tena ndege za shirika hilo.