Habari
Brazil:46 wafariki kwa maporomoko yaliyosababishwa na mvua kubwa
Watu 46 wafariki katika maporomoko ya ardhi yaliosababishwa na mvua kali zilizonyesha nchini Brazil. Nyumba zaidi ya 20 zimekwenda na maji na watu 28 hawajulikani walipo
Mvua kali zilizonyesha nchini Brazil zimepelekea maporomoko ya ardhi ambayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu
Kiongozi wa Kitengo kinachohusika na Usalama wa Rais katika eneo hilo amewatahadharisha wakazi wa maeneo tofauti na mvua kali ambazo zimeripotiwa kuendelea kunyesha. Siku tatu za maombolezo zimetangazwa katika Jimbo la Minas Gerais na katika Miji mingine 47
Na Jacquiline Ngoya