Burudani
Lupita Nyong’o ashinda tuzo ya Oscar ya ‘Best Supporting Actress’
Muigizaji wa Kenya, Lupita Nyong’o Alfajiri ya leo ameshinda tuzo ya Oscar ya muigizaji bora msaidizi wa kike kwa uhusika wake kama Patsey kwenye filamu ya 12 Years a Slave.
Nyong’o, 31, aliyeshinda tuzo ya Oscar kwenye filamu yake hiyo ya kwanza alipata shangwe za nguvu baada ya kutajwa kuwa mshindi.
Lupita akiwa kwenye red carpet ya Oscar
Amemshinda muigizaji mwenzie Jennifer Lawrence wa American Hustle” aliyekuwa akitajwa zaidi kuichukua tuzo hiyo. “Yes!” muigizaji huyo alisikika akisema wakati akipokea tuzo hiyo huku akimkumbatia kaka yake, muongozaji wa 12 Years a Slave, Steve McQueen na waigizaji wengine wa filamu hiyo.
Tuzo hiyo inamweka Lupita kwenye nafasi ya juu kabisa ya mafanikio kwenye Hollywood.