Habari
BREAKING: Mbunge wa CHADEMA Arumeru Mashariki, Joshua Nassari avuliwa ubunge na Spika Ndugai
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amemuandikia barua Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage kumtaarifu kuwa jimbo la Arumeru Mashariki linaloongozwa na Mhe. Joshua Nassari (CHADEMA) liko wazi, kutokana na mbunge huyo kupoteza sifa ya kuwa Mbunge kwa kutokuhudhuria vikao vya mikutano 3 ya bunge mfululizo.
Soma zaidi taarifa iliyotolewa leo na Spika Ndugai.