Bongo5 Exclusives
Breaking News: Bongo Movie Star Cloud Mahututi.
Msanii wa Bongo Movie, Issa Mussa, almaarufu kwa jina la ‘Cloud 112’ amelazwa katika hospitali ya Al Ijumaa iliyopo kariakoo jijini Dar es salaam.
Habari zinasema kwamba Cloud ameugua ghafla akiwa nyumbani kwake ambapo alikimbizwa hospitali hapo kwa ajili ya matibabu.
Mapaka sasa msanii huyo hajapata muafaka wa kinachomsumbua, na Bongo5 ilipomtembelea hospitalini hapo mchana huu,Cloud alishapata majibu ya vipimo vya malaria na kukutwa hana, na Blood pressure ikiwa vile vile ikiwa sawa.
Msanii huyu anasifika kwa ustadi wake wa kisanii hasa katika filamu kama ‘Basilisa, ambapo kipaji chake kinajionyesha dhahiri bila upinzani.
Tunamuombea Cloud apate afueni mapema iwezekanavyo.