Breaking: Watu wasiojulikana wafyatua risasi na kumteka mfanyakazi wa shirika la misaada nchini Kenya
Kundi la watu wasiojulikana waliojihami wamemteka mwanamke mfanyakazi wa shirika la misaada, raia wa Italia kutoka kusini mashariki mwa Kenya, Polisi inasema.
Wanaume hao wanaoarifiwa kujihami kwa bunduki, “wamefyetua risasi kiholela” kabla ya kumteka msaidizi huyo mwenye umri wa miaka 23 kutoka mji wa pwani Malindi.
Watu watano pia wanaarifiwa kujeruhiwa na wamepelekwa hospitalini, mmoja kati yao akiwa yuko katika hali mahututi.
Haijajulikana wazi ni kwanini shambulio hilo limetokea na waliolitekeleza ni akina nani, polisi wanasema.
5 injured, Italian volunteer kidnapped following an attack by armed gunmen in Chakama town, Malindi. The 23 year old works as a volunteer for an NGO in the area. A 10 year old boy is among the injured.
Police have launched a manhunt for the attackers #DayBreak #Malindi #Chakama pic.twitter.com/cKiNGqFjEN— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) November 21, 2018
Hatahivyo, polisi imeeleza kwamba wanalichukulia tukio hilo, lililotokea mwendo wa saa mbili Jumanne usiku kama la kigaidi.
Katika ujumbe kwenye Twitter, idara ya Polisi nchini imesema wanaume hao walikuwa wamebebea bunduki aina ya AK47 walizozitumia kulivamia jumba la kibiashara la Chakama katika kaunti ya Kilifi pwani ya Kenya nje kidogo ya mji wa Malindi.
Polisi kwa sasa wametawanywa kuwasaka wahalifu hao.
The National Police Service wishes to inform the public that last evening at about 8pm, a gang of men armed with AK 47 rifles attacked Chakama Trading centre in Chakama, Makongeni sub location in Kilifi county, about 80 kilometres west of Malindi town. 1/6
— National Police Service-Kenya (@NPSOfficial_KE) November 21, 2018
https://twitter.com/KTNKenya/status/1065125061840068608