Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron kujiuzulu
Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron ametangaza atajiuzulu wadhifa huo October mwaka huu.
Amechukua hatua hiyo baada ya Waingereza wengi kupiga kura ya kujiondoa kwenye umoja wa Ulaya, EU. Cameron amesema amekubali uamuzi wa zoezi aliloliita la demokrasia kubwa.
Cameron na mke wake Samantha
Akiwa na mke wake, Samantha huko Downing Street, Cameron amesema amejivunia kuwa waziri mkuu kwa miaka sita.
Mrs Cameron
Lakini amesema isingekuwa sahihi yeye kuendelea kuwa ‘nahodha wa meli’ kama UK imeamua kujiondoa EU.
“Huu si uamuzi niliochukua kirahisi lakini naamini kuwa ni kwaajili ya faida ya taifa kuwa na muda wa umadhubuti na kisha utawala mpya unahitajika,” alisema huku akilengwa na machozi.
Upande wa kambi ya Leave Campaign ni furaha tu lakini.