Habari
Bruno Mars ampoteza mama yake mzazi weekend hii
Ikiwa ni siku chache toka rapper wa kundi la Outkast Andree 3000 kumpoteza mama yake, mwanamuziki mwingine kutoka Marekani Bruno Mars amefiwa na mama yake mzazi.
Kifo cha mama huyo aitwaye Bernadette Hernandez kimetokea ghafla siku ya Jumamosi (June 1) na amefariki akiwa na umri wa miaka 55.
Mama yake Bruno Mars Hernandez alikuwa ni dancer na muimbaji pia.
Mars alikuwa anategemea kuanza tour yake ya U.S mwezi huu lakini haijafahamika kama kuna mabadiliko ya ratiba ya show hizo kutokana na msiba ulimkuta.